Wednesday, April 9, 2014

REDIO MPYA DAR 93.7 YAWANYIMA WATU USINGIZI..JE NI KWELI NI YA LADY JAY DEE?

Miezi ikapita, mawiki yakasonga hatimae siku, masaa na dakika zake zikapotea na sasa EFM inayopatikana katika masafa ya 93.7 imesikika hewani kwa majaribio kwa mara ya kwanza.

Redio hii iliobeba watangazaji mahiri, waandaaji wa vipindi wenye umakini, ma DJ wanao sadikiwa kuwa walishushwa kwa ajili ya kazi hii, uongozi thabiti na yenye usikivu mujarab, habari zake zilianza kupenya kwenye masikio ya washashi mwishoni mwa mwaka jana na kupelekea wamiliki na wadau wa redio nyengine kukosa usingizi na hata siku wakiupata basi huweweseka usiku na kupiga mayowe ama kujikuta wakikosa hata nguvu ya kuzuia haja ndogo kutoka.

Redio hii itadili kwa asilimia 85 na burudani...na watakaoongoza balaa hilo ni watu wenye kulijuwa game kwa kipindi kirefu saana na burudani iliolengwa hapa hakika ndio mwiba mchungu utaowatesa weengi waliowanyonya na kuwanyanyasa wasanii kwa miongo kadhaa sasa.
Kuna Minong'ono kuwa inamilikiwa na Lady Jay Dee....Kwa mwenye Ukweli Funguka Hapa basiiiii....

Nanga ndio imeshainuka, Unyonyaji ndio umekwisha, Wanyonge mtafarijika, Game sasa litabadilika, Walio Vilaza wataaibika, makini watasikika, Sina imani nina hakika.

0 comments:

Post a Comment